Saturday, March 9, 2013

Waziri Kabaka azindua michuano ya NSSF Media Cuo 2013

Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka (wa pili kushoto), akipiga mpira kuzindua mashindano ya NSSF Media Cup 2013, yanayodhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwenye viwanja vya Sigara, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini na Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Dkt. Ramadhan Dau wa tatu kulia.
 Kikosi kamili cha timu ya soka ya Changamoto kilichowafunga Habari Zanzibar mabao 3-0 leo
 Timu ya Mlimani TV iliyobigizwa bao 46-1
Mchezaji wa timu ya Netiboli ya NSSF. Zamaradi Nzowa (katikati), akijaribu kuwapita wachezaji wa timu ya Mlimani, wakati wa mchezo wa ufunguzi wa michuano ya NSSF Media Cup, inayodhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwenye viwanja vya Sigara, Dar es Salaam leo. NSSF ilishinda 46-1

 Kikosi cha Habari Zanzibar kilichobugizwa mabao 3-0 Uwanja wa Sigara Dar es Salaam leo.
Timu ya Netiboli ya NSSF iliyowagalagaza Mlimani TV mabao 46-1

No comments:

Post a Comment