Wednesday, March 20, 2013

NSSF NA KASI YA UJENZI WA DARAJA LA KIGAMBONI

Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi Karim Mataka (kushoto) akimweleza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Dkt. Ramadhan Dau (katikati) maendeleo ya ujenzi wa Daraja hilo, linalojengwa kwa ushirikiano wa Serikali na NSSF, Dar es Salaam jana Wa pili kulia ni Meneja Kiongozi wa Mradi huo Mhandisi John Msemo na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu kulia.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt Ramadhan Dau na maofisa kutoka Shirika hilo, wakitembelea mradi wa ujenzi wa daraja hilo Dar es Salaam jana.
Sehemu ya daraja la muda lililojengwa kwa ajili ya kupitisha vifaa vya ujenzi wa daraja la kisasa la Kigamboni Dar es Salaam
 Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja hili Mhandisi John Msemo (kulia) wa NSSF akiwa na Bw. Abdallah Mseri wakitembelea mradi huo jana.
Vifaa vya ujenzi vikiendelea kufanya kazi kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la kisasa la Kigamboni.
Maofisa kutoka NSSF wakijadiliana jambo eneo la mradi wa ujenzi wa daraja hilo.
 Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni Mhandisi John Msemo akimuonyesha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt Ramadhan Dau jinsi mafundi wanavyomwaga zege wakati wa ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam jana.

Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja hilo, Mhandisi Karim Mataka akiwa katika mavazi ya kazi eneo la ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam jana.

No comments:

Post a Comment