Wednesday, March 20, 2013

KAMATI YA BUNGE YATEMBELEA UJENZI DARAJA LA KIGAMBONI

 Naibu Waziri wa Ujenzi, Bw. Gerson Lwenge (wa tatu kulia), akiwa na maofisa wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii wakiwasubiri Wabunge wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, waliotemebea mradi wa ujenzi daraja la Kigamboni, Dar es Salaam jana.
 Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kisasa la Kigamboni, Mhandisi John Msemo (aliyesimama), akitoa ufafanunuzi kuhusu ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam jana
 Wabunge wa Kamati ya Miundombinu wakifuatilia maelezo ya Mhandisi Msemo kwa makini.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhan Dau akiwakaribisha Wabunge wa Kamati ya Miundombinu, walipotembelea mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bw. Peter Selukamba.


 Maendeleo ya ujenzi wa daraja la Kigamboni.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt Ramadhan Dau (wa tatu kushoto) na Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, Mhandisi John Msemo (kushoto) wakiwaongoza Wabunge wa Kamati ya Miundombinu kukagua mradi wa ujenzi wa daraja hilo Dar es Salaam jana.
Dkt Ramadhan Dau (kulia) na Mhandisi John Msemo (katikati), wakimuonyesha Mwenyekiti wa Kamati ya Miondombinu, Bw. Peter Selukamba, mahali ambapo daraja hilo litapita baada ya kukamilika na kuanza kupitika.
 Mafundi wakiendelea na ujenzi wa daraja hilo
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja hilo kutoka NSSF, Mhandisi John Msemo (kushoto), akiwatembeza Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu Bw. Peter Selukamba (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara TANRODS, Mhandisi Patrick Mfugale, walipotembelea mradi wa ujenzi wa daraja hilo jana.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la kisasa la Kigamboni wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi John Msemo (kulia), akitoa ufafanuzi wa ujenzi wa daraja hilo kwa Wabunge wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walipotembelea mradi huo Dar es Salaam jana.
 Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt. Dau akitoa ufafanuzi kuhusu mradi wa ujenzi wa daraja hilo.

Mhandisi Karim Mataka(kushoto) akiteta na Maofisa Waandamizi wa Idara ya Uhusiano ya NSSF, Juma Kintu (kulia) na Teopista Mheta.

No comments:

Post a Comment