Naibu Waziri wa Ujenzi, Bw. Gerson Lwenge (wa tatu kulia), akiwa na maofisa wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii wakiwasubiri Wabunge wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, waliotemebea mradi wa ujenzi daraja la Kigamboni, Dar es Salaam jana.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kisasa la Kigamboni, Mhandisi John Msemo (aliyesimama), akitoa ufafanunuzi kuhusu ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam jana
Wabunge wa Kamati ya Miundombinu wakifuatilia maelezo ya Mhandisi Msemo kwa makini.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhan Dau akiwakaribisha Wabunge wa Kamati ya Miundombinu, walipotembelea mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bw. Peter Selukamba.
Maendeleo ya ujenzi wa daraja la Kigamboni.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt Ramadhan Dau (wa tatu kushoto) na Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, Mhandisi John Msemo (kushoto) wakiwaongoza Wabunge wa Kamati ya Miundombinu kukagua mradi wa ujenzi wa daraja hilo Dar es Salaam jana.
Dkt Ramadhan Dau (kulia) na Mhandisi John Msemo (katikati), wakimuonyesha Mwenyekiti wa Kamati ya Miondombinu, Bw. Peter Selukamba, mahali ambapo daraja hilo litapita baada ya kukamilika na kuanza kupitika.
Mafundi wakiendelea na ujenzi wa daraja hilo
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja hilo kutoka NSSF, Mhandisi John Msemo (kushoto), akiwatembeza Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu Bw. Peter Selukamba (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara TANRODS, Mhandisi Patrick Mfugale, walipotembelea mradi wa ujenzi wa daraja hilo jana.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la kisasa la Kigamboni wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi John Msemo (kulia), akitoa ufafanuzi wa ujenzi wa daraja hilo kwa Wabunge wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walipotembelea mradi huo Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt. Dau akitoa ufafanuzi kuhusu mradi wa ujenzi wa daraja hilo.
Mhandisi Karim Mataka(kushoto) akiteta na Maofisa Waandamizi wa Idara ya Uhusiano ya NSSF, Juma Kintu (kulia) na Teopista Mheta.
Wednesday, March 20, 2013
NSSF NA KASI YA UJENZI WA DARAJA LA KIGAMBONI
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi Karim Mataka (kushoto) akimweleza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Dkt. Ramadhan Dau (katikati) maendeleo ya ujenzi wa Daraja hilo, linalojengwa kwa ushirikiano wa Serikali na NSSF, Dar es Salaam jana Wa pili kulia ni Meneja Kiongozi wa Mradi huo Mhandisi John Msemo na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu kulia.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt Ramadhan Dau na maofisa kutoka Shirika hilo, wakitembelea mradi wa ujenzi wa daraja hilo Dar es Salaam jana.
Sehemu ya daraja la muda lililojengwa kwa ajili ya kupitisha vifaa vya ujenzi wa daraja la kisasa la Kigamboni Dar es Salaam
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja hili Mhandisi John Msemo (kulia) wa NSSF akiwa na Bw. Abdallah Mseri wakitembelea mradi huo jana.
Vifaa vya ujenzi vikiendelea kufanya kazi kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la kisasa la Kigamboni.
Maofisa kutoka NSSF wakijadiliana jambo eneo la mradi wa ujenzi wa daraja hilo.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni Mhandisi John Msemo akimuonyesha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt Ramadhan Dau jinsi mafundi wanavyomwaga zege wakati wa ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam jana.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja hilo, Mhandisi Karim Mataka akiwa katika mavazi ya kazi eneo la ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt Ramadhan Dau na maofisa kutoka Shirika hilo, wakitembelea mradi wa ujenzi wa daraja hilo Dar es Salaam jana.
Sehemu ya daraja la muda lililojengwa kwa ajili ya kupitisha vifaa vya ujenzi wa daraja la kisasa la Kigamboni Dar es Salaam
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja hili Mhandisi John Msemo (kulia) wa NSSF akiwa na Bw. Abdallah Mseri wakitembelea mradi huo jana.
Vifaa vya ujenzi vikiendelea kufanya kazi kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la kisasa la Kigamboni.
Maofisa kutoka NSSF wakijadiliana jambo eneo la mradi wa ujenzi wa daraja hilo.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni Mhandisi John Msemo akimuonyesha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt Ramadhan Dau jinsi mafundi wanavyomwaga zege wakati wa ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam jana.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja hilo, Mhandisi Karim Mataka akiwa katika mavazi ya kazi eneo la ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam jana.
Saturday, March 9, 2013
NJAMA
SURA YA TISA
MAPAMBANO NA VIBARAKA
Ilikuwa saa kumi na mbili na nusu za asubuhi wakati nilipokuwa nakaribia kumaliza kunyoa ndevu. Nilikiangakia kidevu changu kwenye kioo nikaona nilikuwa sijajinyoa vizuri. Kila wakati nilipokuwa na mawazo mengi kitu kama hiki kilikuwa kinanitokea . Lakini hata hivyo nia yangu nionekane nadhifu hivyo nilichukua tena mashine ya ndevu na kuanza kujinyoa. Nilipoona mambo yanakuwa mazuri kwenye kidevu changu, nikaanza kuoga.
Nilitoka maliwatoni na kurudi chumbani nilikokuwa nimelala. Zabibu bado alikuwa hajaamka, hivyo nilivaa taratibu ili nisije nikamshtua toka usingizini. Alikuwa na sura ya mtoto mchanga isiyokuwa na maneno. Nilimwangalia huku nikivaa. Nilipomaliza kuvaa na kuweka kila kitu changu tayari, nilikwenda nikambusu Zabibu usingizini nikaondoka ndani ya chumba na kufunga mlango taratibu.
Niliwakuta Sherriff na Eddy wamekaa sebuleni wanakunywa kahawa.
"Karibu bosi, habari za kuamka?".
"Nzuri", nilijibu, nikaa kwenye kiti cha meza ya kulia nikavuta kikombe cha chai na kujiwekea kahawa ya kutosha.
"Lazima iwe nzuri", Sherriff alijibu huku akitabasamu nikajua alikuwa na maana gani kusema hivyo.
"Usinionee wivu".
"Lazima tukuonee wivu, maana chuma kama hicho si cha kawaida.
"Bosi, vijana wameleta habari kama ulivyoomba", Eddy alisema huku akibadilisha mazungumzo.
"Ndio, wamesemaje.
"Wamesema hawakuweza kumwona Sikazwe mpaka saa tisa za usiku. Walimpata akitokea kwenye barabara ya Bagamaoyo na akielekea nyumbani kwake. Hawakuweza kujua alikuwa anatokea wapi. Na mpaka sasa hivi bado yuko nyumbani amelala. Wamenieleza kuwa ofisi za SANP hazifanyi kazi siku za Jumamosi. Na kama unavyojua leo ni Jumamosi".
"Basi waambie waendelee na wahakikishe kuwa hawapotezi hata dakika moja. Atakapoondoka nyumbani nataka kujua anaelekea wapi. Sawa?".
"Hamna taabu".
"Sasa hivi mimi ninakwenda kumwona Chifu maana nilipata habari kuwa anataka ripoti toka kwangu, maana anasumbuliwa sana na Serikali".
"Nafikiri Sherriff anaweza kuendelea kupumzika hapa, mimi nitakujulisha wakati nitakapokuhitaji".
"Sawa", alijibu Sherriff kwa mkato.
"Naomba unipatie 'machine gun' inayoweza kuchukua risasi zaidi ya mia. Niliwahi kuzitumia nilipokuwa jeshini.
"Aina gani".
"Zilizotengenezwa Urusi".
"Zipo".
"Oke niletee moja ya aina hiyo. Ikiwezekana tuma mtu aniletee mapema kusudi niishughulikie".
"Hamna taabu, utapata.
Baada ya kuzungumza na hawa vijana tuliagana kisha nikaondoka. Nilitembea kwa mguu mpaka nyumbani kwangu, ili nikabadilishe nguo. Nilifika nikafungua mlango, nikaangalia saa yangu nikaona ilikuwa yapata saa mbili kasoro robo. Nilipoingia tu ndani, roho yangu ikashtuka lakini nilikuwa nimechelewa, nilipigwa na mfuko wa mchanga kisogoni nikaanguka.
II
Nilisikia sauti ikisema ni saa tisa sasa. Sauti hiyo ndiyo ilikuwa imenizindua. Nilijikuta nimelazwa kwenye kitanda cha chuma bila godoro, na nilijikuta nimefungwa kwenye kitanda mikono na miguu. Kichwa kilikuwa kinaniuma sana, na kwa chati nilifunua nilikuta nimo kwenye chumba kidogo cha giza tupu.
Nikatuliza mawazo nikaanza kufikiri nini kimetokea. Ndipo nikatambua kuwa nilipokuwa nakwenda nyumbani kwangu saa mbili kasorobo nilipigwa na kitu nilichohisi ni mfuko wa mchanga nikaanguka chini. Tokea hapo mpaka sasa sikujua chochote. Hii ina maana kuwa nilizimia. Nikakumbuka yule mtu alisema ilikuwa saa tisa, hii ina maana nilikuwa nimezimia kwa zaidi ya masaa sita.
Nilifikiri jinsi akina Eddy, Sherriff, zabibu na Chifu walivyokuwa wamehangaika huu kujaribu kunitafuta. Hata mimi mwenyewe nilikuwa sijui hapa ni wapi. Ila nilikuwa nasikia kelele nyingi nje ya chumba hiki. Hivyo nilifikiri kuwa huenda ikawa ni sehemu ya viwanda. Sikujua ile sauti iliyosema sasa ni saa tisa ilitokea wapi, maana kulionekana kana kwamba hakukuwa na mtu ndani ya chumba hiki.
"Zaidi ya saa tisa sasa lazima waje kutupokea sisi twende tukapate chochote", nilisikia tena mtu anazungumza.
"Washa taa", sauti nyingine ikajibu.
Hivyo nikajua kuwa nilikuwa nalindwa na watu wawili ila sikuweza kuwaona kwa sababu ya giza. Taa ilipowashwa mimi nikajifanya kana kwamba bado nimezimia kabisa.
"Bado kazimia kabisa", alisema mmoja wao.
"Daktari alisema hawezi kuamka mpaka saa kumi na mbili au baada ya hapo", alijibu mwingine.
"Kama ni hivyo basi twende tukawaambie watupokee njaa inauma sana".
"Oke twende, zima taa".
Walifungua mlango na kuzima taa halafu wakafunga mlango na funguo wakaondoka. Mimi nilijinyanyua ili nione nimefungwa kiasi gani. Nilikuta ni mikono na miguu tu iliyofungwa kwenye kitanda cha chuma kipatacho futi tatu upana. Miguu ilifungwa kwa ustadi sana kiasi kuwa nilisikia kama damu haipiti na sehemu za nyayo zimekufa ganzi. Kwa upande wa mikono, mkono wa upande wa ukutani nilipoujaribu nikaona haukufungwa kwa ustadi sana, ule wa upande mwingine ndio ulifungwa kwa ustadi sana.
Nilinyanyua kichwa changu nikasikia kinauma sana, nikakirudisha chini. nilianza kufikiri namna gani nitajiokoa. Baada ya kufikiri sana nikaona njia pekee ni kujaribu kufungua hizi kamba kabla walinzi hawa hawajarudi. Hivyo nilionelea nijikaze. Ingawaje kichwani nilisikia maumivu makali. Kwa vile sehemu zote tokea tumbo, kifua na kichwa zilikuwa hazikufungwa, na kitanda kilikuwa cha futi tatu nilijikunja ili mdomo wangu ufikie kamba za mkono wa upande wa ukutani ambao haukuwa umefungwa sana.
Nilitulia tena nikamwomba Mungu. Niliupeleka mdomo wangu kwenye fundo la kamba walilokuwa wamenifungia. Kwa bahati mdomo wangu ulifika nikaanza kupitisha meno yangu kwenye kamba ili niweze kujua wamefungaje. Katika hii tafuta tafuta huku maumivu karibu yananitoa fahamu, niliuma ncha moja ya kamba, nikaivuta na fundo lote la kamba likafunguka na mkono wangu wa kulia ukawa huru.
Ilibidi nirudishe kichwa changu kipumzike maana maumivu yangu yangeweza kunifanya nizimie.
Nikiwa na mkono mmoja huru, nilipata tumaini na nguvu mpya. Nilichoomba sasa ni watu hawa wasije upesi. Kwa vile walikuwa wamesema daktari aliwaambia siwezi kuamka kabla ya saa kumi na mbili nilijua watadharau kuja ndani ya chumba hiki cha joto la kuweza kuua kabla haijakaribia saa kumi na mbili wakati wananitegemea kuamka. Nguvu mpya zilizoletwa na mawazo kuwa nimechelewa mambo mengi zilinifanya nisahau kabisa maumivu yangu.
Niliutumia mkono wangu wa kulia kufungua mkono wa kushoto. Nikiwa sasa nimeweza kufikia hatua hii niliingiwa na furaha nikaanza kushambulia kamba nilizofungwa miguuni. Kwa mtu mwenye ujuzi kama wangu hii haikunipa taabu na mara nikawa huru tayari kupambana na wadhalimu hawa.
Nilirudi nikajilaza nikaziweka kamba kijanja kana kwamba bado hazijafunguliwa. Nikawa katika hali ya kusubiri. Nilivyokuwa na bahati haikupita muda mrefu nikasikia funguo zinaingia ndani ya kufuri la mlango. Mara mlango ukafunguliwa na taa zikawashwa. Mimi nilijilaza vile vile na kujifanya bado nimezirai.
"Bado sana huyu, niliwaambia daktari alisema saa kumi na mbili. Angekuwa mtu wa hivi hivi asiye na mazoezi pigo lile lingemuua pale pale", nilisikia sauti ikisema.
"Sawa. Akiamka saa kumi na mbili itakuwa vizuri maana ndipo wakati wazee watakapomhitaji", sauti nyingine ilijibu.
"Haya shika funguo, mwangalie kwa makini akionyesha dalili ya kupata fahamu tupashe habari mara moja. Sisi tuko chumba kingine tukisubiri maelekezo zaidi kutoka kwa wazee.
"Haya asante, lakini naomba asiamke wakati nikiwa peke yangu. Nasikia mtu huyu ni hatari kubwa kabisa'.
"Wewe mwoga sana. Mtu aliyefungwa kiasi hiki unafikiri atafanya nini hata akiamka, labda awe na nguvu za kishetani".
"Huenda anazo".
"Kama anazo basi pole, yatakuwa matatizo yako".
Nikiwa katika kusikiliza mazungumza haya kidogo nicheke. Yule mtu mwingine alitoka, akabaki mlinzi mmoja ambaye alifunga mlango na kuzima taa, halafu akakaa kwenye kiti. Nilisubiri kama dakika kumi hivi nikaanza kukoroma. Yule mlinzi aliinuka na kuwasha taa na kunisogelea kitandani wakati mimi bado nimefumba mamcho. Kule kuhema kwake ndiko kulinifanya nijue yuko karibu.
"Wewe umeamka", aliuliza kwa wasiwasi, nilifungua macho yangu kwa chati nikaona alikuwa ameshika bastola akiwa amelenga kifuani pangu. Nilifanya mahesabu ya namna ya kumwingia mtu huyu nikapata.
"Ndiyo', nilijibu kwa unyonge.
Niliona macho yanamtoka, nikaona mtu huyu ameingiwa na woga na anaweza kunipiga risasi shauri ya woga nisipomwahi. Hivyo kama chui nilimrukia na wakati ule ule nikawa nimepiga bastola yake ikaanguka upande mwingine na nikampiga pigo la mkono la karate katikati ya kichwa akafa bila kujua nini kimemwua. Niliiendea bastola yake, nikamvua joho lake jekundu, nikalivaa, kisha nilifungua bastola nikakuta funguo na risasi za bastola hii. Nilifungua bastola nikakuta ina risasi tatu tu nayo ina uwezo wa kubeba kumi. Hivyo niliijaza risasi, kisha nikachemsha kidogo viungo vyangu tayari kwa kupambana na watu walioko chumba kingine. Kichwa kilikuwa bado kinaniuma lakini hakikuwa tishio kubwa.
Nilizima taa, nikajaribu kufikiri nilipo lakini nikaona bila kwenda nje haingenisaidia. chumba hiki kilionekana kilikuwa ni stoo ya vitu, hivyo nilihisi hapo nje kuna ofisi na nilifikiri kuwa ndicho chumba cha pili alichokuwa amezungjumzia yule mlinzi wa pili. Nilifungua mlango taratibu, niliangalia hali mara moja nikajua hizi zilikuwa sehemu za nyuma za bohari, au ofisi. Maana kulikuwa na chumba kinatazamana na stoo hii, halafu kulikuwa na vyumba vitatu mbele tena kwa upande wa kulia. Upande wa kushoto kulikuwa na mlango wa kutokea uwani.
Nilisikia watu wanazungumza kwenye chumba kilichokuwa kinaangaliana na mahabusu yangu. Nikajua ni hiki chumba alichozungumza yule mlinzi. Nilijiweka tayari kisha nikagonga. Mimi niliamini watajua ni mwenzao hivyo wangekuja bila tahadari kufungua mlango.
"Ngwishe", nilisikia sauti ikiita.
"Ndiyo", nilijibu kwa sauti nzito.
"Ameamka?".
"Bado".
"Funguo tu mlango haukufungwa", nilijibiwa.
Basi bastola yangu ikiwa tayari mkononi, nilifungua mlango na kuingia ndani. Kweli watu wote sita walikuwa wamwezunguka meza wanakula. Waliponiangalia na kunitambua mimi ni nani wengine chakula kiliwadondoka toka midomoni.
"Endeleeni kula, mbona mnaacha", niliwatania.
Mmoja wao alimkonyeza mwenziwe wakifikiri mimi sikuona kumbe hawakujua macho ya Willy yamefundishwa kuangalia kila mahali kwa wakati mmoja utafikiri kinyonga. Yule aliyekonyezwa alitoa bastola haraka sana lakini mimi nilijua anataka kufanya nini na kabla hata sijamtahadhalisha alikuwa tayari kufyatua, lakini mimi nilikuwa mwepesi zaidi nikampata. Wakati yeye alipofyatua risasi alimpiga mwenzake na kumwua. wawili tayari walikuwa wamekufa.
Pale pale wengine wote walisimama kila mtu akitoa bastola. Lakini niliwawahi watatu halafu nikaona yule wa nne macho yake yanaangalia mlango. Mara moja nikaanguka chini na risasi ikanikosa kwa nyuma ikapita na kumpiga yule wa nne na kummaliza, mimi pale pale nikajiviringisha na kumwahi yule wa nje. Lo nilikuwa nimeponea chupu chupu, maana kama nisingewahi kulala chini, vile vile ningekwenda kuonana na Veronika mpenzi wangu kama kweli watu huwa wanaonana tena huko ahera.
Nilitoka ndani ya jengo hili upesi upesi. Nilipofika nje nikaona niko kwenye mabohari ya Chang'ombe. Bohari hii ilikuwa imezungukwa na ua wa matofali. Nilivua joho jekundu nikapanda ua nikatokea katika uchochoro nikaanza kukimbia. Nilikadilia kuwa ilikuwa yapata saa kumi na moja. Nilipofika mbele ya bohari nilikuta ni mali ya Kampuni moja ya matairi ya magari iitwayo "Trans World Tyres", kwa sababu sikutaka kufanya uchunguzi zaidi kutokana na hali niliyokuwemo niliona teksi nikaipungia ikasimama na kumwamuru dereva anipeleke Independence Avenue haraka.
ITAENDELEA
Waziri Kabaka azindua michuano ya NSSF Media Cuo 2013
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka (wa pili kushoto), akipiga mpira kuzindua mashindano ya NSSF Media Cup 2013, yanayodhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwenye viwanja vya Sigara, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini na Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Dkt. Ramadhan Dau wa tatu kulia.
Kikosi kamili cha timu ya soka ya Changamoto kilichowafunga Habari Zanzibar mabao 3-0 leo
Timu ya Mlimani TV iliyobigizwa bao 46-1
Mchezaji wa timu ya Netiboli ya NSSF. Zamaradi Nzowa (katikati), akijaribu kuwapita wachezaji wa timu ya Mlimani, wakati wa mchezo wa ufunguzi wa michuano ya NSSF Media Cup, inayodhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwenye viwanja vya Sigara, Dar es Salaam leo. NSSF ilishinda 46-1
Kikosi cha Habari Zanzibar kilichobugizwa mabao 3-0 Uwanja wa Sigara Dar es Salaam leo.
Timu ya Netiboli ya NSSF iliyowagalagaza Mlimani TV mabao 46-1
Kikosi kamili cha timu ya soka ya Changamoto kilichowafunga Habari Zanzibar mabao 3-0 leo
Timu ya Mlimani TV iliyobigizwa bao 46-1
Mchezaji wa timu ya Netiboli ya NSSF. Zamaradi Nzowa (katikati), akijaribu kuwapita wachezaji wa timu ya Mlimani, wakati wa mchezo wa ufunguzi wa michuano ya NSSF Media Cup, inayodhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwenye viwanja vya Sigara, Dar es Salaam leo. NSSF ilishinda 46-1
Timu ya Netiboli ya NSSF iliyowagalagaza Mlimani TV mabao 46-1
NJAMA
SURA YA NANE
BINTI TANZANIA
III
Tulipofika nyumbani kwa Eddy ilikuwa saa tano za usiku. Tuliingia tukaa kwenye viti. Eddy akaleta vinywaji.
"Kifo cha Veronika kimeniuma sana, tokea sasa mimi nimeahidi nitakuwa bega kwa bega na wewe mpaka nione mwisho wa mambo haya", Sherriff aliniambia huku machozi yakimtoka.
"Sijui nikwambie nini Sherriff, maana hali niliyonayo mimi siwezi kuieleza. Afadhali tuiachie hapo hapo".
"Basi, mambo yote tumetengeneza. Chifu amesema mwili wa Veronika hauwezi kusafirishwa mpaka mwisho wa mambo yote ili aweze kupewa heshima zote za kijeshi. Hivyo mwili wake umetunzwa huko kwenye chumba cha maiti katika hospitali ya Muhimbili mpaka hapo tutakapojua mwisho wa mambo haya. Mwili wake utapewa uangalizi wa pekee hivyo hata tukichukua mwezi mzima utakuwa katika hali safi tu", Eddy alieleza.
"Jambo hili haliwezi kuchukua siku mbili zaidi. Nimeshapata mwanga mkubwa wa kutosha. Kuna kitu kidogo tu ambacho bado kinakosekana lakini naamini kesho haiishi bila kukupata kitu hicho", niliwaeleza. Kisha nikawaeleza jinsi nilivyokuwa ninafikiria mambo yalivyo toka mwanzo mpaka mwisho.
"Sasa ninachotafuta ni yale magari waliyapata wapi?.Nguo ni rahisi pamoja na vyeo kama nilivyowaeleza. nikishajua hilo basi jambo hili tutakuwa tumelitatua. Itabaki sasa kufanya shughuli ya mwisho ambayo ni kuzikamata hizi silaha na kuwakamata vibaraka hawa".
Wote walitingisha vichwa kuonyesha wamenielewa.
"Ray Sikazwe anakaa wapi?", nilimwuliza Zabibu.
"Anakaa Oysterbay, Kenyata Drive nyumba Nambari 1000/D.
"Oke, Eddy tokea sasa hivi weka vijana wa kumfuata Ray Sikazwe kila mahali anapokwenda. Ifikapo asubuhi nataka nataka nijue nyendo zake zote na sisi tutawasaidia tokea hapo. Tukiweza kufanya hivyo kazi itakuwa rahisi. Baada ya mambo yote yaliyotokea leo lazima akipata habari atakuwa na wasiwasi, hivyo lazima tu atafanya kitu cha kujinasa. Wote tutalala hapa maana ndiko mahali hapafahamiki.
"Tutaonana asubuhi", niliwaaga.
Nyumba ya Eddy ilikuwa na vyumba vitatu vya kulala. Kwa vile Zabibu alikuwa na huzuni nyingi na kwa vile mimi pia nilikuwa na huzuni tulionelea afadhali tukalala pamoja ili tuweze kuliwazana mioyo.
ITAENDELEA
Friday, March 8, 2013
Michuano ya NSSF Media Cup kutimua vumbi kesho
Meneja Uhusiano na Huduma kwa wateja wa Shririka la Taifa la Hifadhi ya Jamii, Eunice Chiume, akizunguma na Waandishi wa Habari Dar es Salaam jana, kuhusu uzinduzi wa michuano ya NSSF Media Cup, inayoanza kwenye viwanja vya Sigara na DUCE Chang'ombe Jijini kesho.
Eunice akimkabidhi jezi kwa mwakilishi wa timu ya NSSF, Linus Bwegoge (kulia)
Eunice Chiume (kushoto), akikabidhi mpira kwa Julius Kihampa wa Jambo Leo kulia. huku Afisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF Juma Kintu akishuhudia.
Enice akikabidhi jezi kwa Joyce Nsima kulia wa Sahara Media
Majuto Omari wa Mwananchi Communication akipokea jezi leo
Vivien Msilu wa Business Times kulia akipokea jezi kutoka kwa Eunice wa NSSF, Dar es Salaam leo
Paul Urio wa IPP akipokea jezi kwa ajili ya timu yake
Ridhwan Ramadhan wa Changamoto akipokea mpira
Chacha Maginga wa TBC akipokea jezi
Mohamed Mharizo wa Habari Communicatin akipokea jezi.
Rashid Zahor wa Uhuru Communication akipokea jezi
Eunice akiongea na wajumbe wa michuano ya NSSF Media Cup 2013
Akisisitiza jambo
Eunice akimkabidhi jezi kwa mwakilishi wa timu ya NSSF, Linus Bwegoge (kulia)
Eunice Chiume (kushoto), akikabidhi mpira kwa Julius Kihampa wa Jambo Leo kulia. huku Afisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF Juma Kintu akishuhudia.
Enice akikabidhi jezi kwa Joyce Nsima kulia wa Sahara Media
Majuto Omari wa Mwananchi Communication akipokea jezi leo
Vivien Msilu wa Business Times kulia akipokea jezi kutoka kwa Eunice wa NSSF, Dar es Salaam leo
Paul Urio wa IPP akipokea jezi kwa ajili ya timu yake
Ridhwan Ramadhan wa Changamoto akipokea mpira
Chacha Maginga wa TBC akipokea jezi
Mohamed Mharizo wa Habari Communicatin akipokea jezi.
Rashid Zahor wa Uhuru Communication akipokea jezi
Eunice akiongea na wajumbe wa michuano ya NSSF Media Cup 2013
Akisisitiza jambo
Wednesday, February 27, 2013
NJAMA
SURA YA NANE
USIKU WA HEKAHEKA
Tulipofika Kilimanjaro Hoteli ilikuwa yapata saa tatu kamili. Tulipokuwa njiani kuelekea Kilimanjaro nilimweleza Eddy mambo yote niliyokuwa nimepata toka kwa Zabibu, mambo ambayo hata yeye alisema yalionyesha ufumbuzi wa jambo hili kwa mtu mwenye kufikiri. Tuliingia hotelini tukapanda lifti iliyotushusha orofa ya pili. Tulipotoka ndani ya lifti mara ile hali ya tahadhari ilituingia. Mimi nilitoa bastola yangu nikaiweka tayari na Eddy akafanya vile vile.
Tulipofika mlango wa chumba namba 206 tulikuta umefungwa, niligonga nikiwa nimesimama upande kabisa. Niligonga mlango mara mbili haraka haraka, halafu nikatulia kidogo kisha nikagonga tena, kwani hivi ndivyo Veronika alikuwa amenielekeza namna ya kujitambulisha lakini sikusikia kitu. Nilimonyesha ishara Eddy abane ukutani wakati mimi nafungua.
Nilifungua mlango ghafla. Tishio nililolikuta sijawahi kulipata tena, kwani Veronika alikuwa amelala kwenye sofa na kisu chenye mpini mwekundu kikiwa kimemwingia juu kidogo ya titi la kushoto. Kidogo ningezimia lakini nilijikaza nikakimbia pale kwenye sofa huku nikikanyaga maiti za watu wengine hapo chumbani.
Veronika alikuwa bado ameshikilia mkono wa simu mikononi mwake. Nilipomfikia nilimkuta bado yuko hai. Wakati huo Eddy nae alikuwa ameingia akanipa glasi ya whiski.
"Bosi jikaze, mnyweshe hii whiski mimi naita gari la hospitali"'
Nilimnywesha Veronika kisha nikamtingisha akafunua macho akapata fahamu kidogo.
"Vero, Willy hapa, niambie nani amefanya hivi".
"Walikuja.... watatu... nikapam...bana ...nikawaua nikakupigia simu.... ku...ku...kumbe walikuwepo... wengine ...wawili ... mmoja ... akamwita ... Shu... Shu...Shuta muue.... mimi kugeuka ... akanichoma... ki... kisu... nikawahi ...kumpiga yule mwingine ...kwa... akafa... Shuta... akakimbia ...nika...
Hakuweza kusema tena. Nikamwongeza whiski na kumtingisha.
"Oh Vero, nimeita gari la wagonjwa na mganga anakuja sasa hivi utapona tu.
"Si...siwezi...nitakufa...nimekufa...ame...moyo...Willy na...nakufa...na...ku...penda ...hakuna tena... mwanamume... niliye... mpenda...kama wewe. Ni...nimefurahi...kukuona ...ma...mara... ya...mwisho...nikifa ...kwa ajili ya Afrika... siogopi...kufa...kwani nimekufa ...kwa sa...sabab...bu...nzuri. Ende...le..za ...ma...pa...mba...no... Willy ...Mungu...a...ku...sai...die...uni...ku...pi...zie...kisasi Afrika. Ni...busu...na... ku...
Nilijua Veronika hawezi kuchukua dakika moja zaidi, niliweka midomo yangu kwenye midomo yake na kulamba damu yake ambayo sasa ilikuwa inatoka mdomoni.Alitabasamu na macho yake yakang'ara kiasi ambacho sikuwahi kuyaona yanang'ara vile halafu akayapepesa akafariki. Alikufa huku akitabasamu.
Sikuwahi kulia na kupata uchungu kama wakati wa kifo cha Veronika. Nilijilaumu. Kama ningekwenda nae kwa Zabibu asingekufa.
Eddy alinikuta nabubujika machozi kama mama anayemlilia mtoto wake wa pekee.
"Bosi jikaze", Eddy alinishauri.
"Washenzi hawa, nduli hawa, watanitambua. Kwanini Mungu anaruhusu mtu kama Veronika kufa mikononi mwangu?. Eee Mungu nisaidie nilipize kisasi kwa ajili ya mwanamapinduzi huyu wa Afrika nzima", niliomba kwa sauti huku machozi yananitoka. Vero alikuwa amekufa kishujaa. Alikuwa amewaua maadui wanne pale pale chumbani.
Niling'oa kile kisu nikasafisha damu yake kwenye nguo zake.
"Kisu hiki hiki kitawauwa kama walivyomwua Veronika", nilisema.
"Bosi ninataka toka sasa tuwe pamoja".
"Hapana sasa hivi, fanya mpango wa kuondoa maiti hizi humu ndani. Na umwarifu Chifu, polisi wala wakuu wa hoteli wasiingilie. Na halafu kampashe Sherriff habari hizi za huzuni. Muushughulikie mwili wa Veronika uweze kupelekwa kwao. Mwambie Sherriff ashughulike na habari hiyo tu mambo mengine aniachie. Mwambie Chifu mambo yote yalivyo mpaka sasa mimi namfuata Shuta lazima alipe. Fanya hayo kwanza halafu nitakapokuhitaji nitakujulisha".
Niliondoka na kumwacha Eddy mle ndani ya chumba nikakimbia kwenye lifti iliyonitelemsha chini. Nilipita pale mapokezi huku nikikimbia kiasi cha watu wote kunishangaa.
Niliingia ndani ya gari Eddy alilokuwa amekodi na kuliacha Kilimanjaro Hoteli nikaondoka kwenda kumtafuta Shuta.
II
Niliondoka na kuelekea nyumbani kwa Eddy nilikomwacha Zabibu. Njiani nilifikiria uhusiano wangu na Veronika tokea siku tuliyoonana mwenye ndege mpaka kifo chake kilipotokea mikononi mwangu dakika chache zilizopita. Nilisikia uchungu usio kifani. Hasira na chuki yangu kwa makaburu, mabeberu na vibaraka wao ilizidi kiwango chake cha kila siku.
"Kifo peke yake ndicho kitaniachisha kuwawinda hawa wadhalimu maishani mwangu", niliapa.
Nilipofika nyumbani kwa Eddy nilimkuta Zabibu amekaa kwenye sofa pale tulipomwacha.
"Kumetokea nini, mbona ulikuwa unalia?", Zabibu aliniuliza baada ya kuniangalia kwa muda mfupi.
Nilimweleza yaliyompata Veronika, na jinsi urafiki wetu na Veronika ulivyokuwa umekomaa tangu kuonana mwenye ndege wakati tukielekea Freetown. Hakika nilijuta kumfahamu Veronika afadhali nisingeonana nae.
"Usisikitike sana, sasa tunakuwa watu wawili tuliopoteza marafiki zetu. Lililopo sasa ni sisi kutiana moyo na kusaidiana kuwatafuta hawa waliofanya matendo haya.
Nilijisikia vizuri kidogo Zabibu kuwa pamoja nami.
"Unajua Shuta anapokaa?", niliuliza.
"Ndio, anakaa Oysterbay, Kaunda Drive No. 11230".
"Basi, sasa wewe tulia hapa mimi nitarudi muda si mrefu".
"Twende sote".
"Hapana. Kazi hii huijui niachie mimi, wewe pumzika hapa. Ukiona usingizi chumba hicho hapo kalale. Tutaonana baadaye".
"Lakini jihadhari inaonekana watu hawa ni hatari kabisa, sitapenda kusikia umeuawa, nikisikia tu na mimi nitajiua", aliniambia Zazibu akionyesha hali ya mapenzi kama kwamba tumekuwa marafiki siku nyingi.
Mimi huwa sielewi kwa nini binadamu hawa hutokea kunipenda mara tu nionyeshapo uso wangu. Niliondoka na kuelekea Oysterbay. Niliingia Kaunda Drive na kuanza kuangalia namba za nyumba. Niliendesha polepole mpaka nikaona nyumba. Nilipokuwa napita mbele ya lango la nyumba hiyo mlango wa mbele ulifunguliwa mimi nikaendelea mbele kidogo nikaegesha gari langu, halafu nikarudi kwa miguu.
Nilipofika kwenye ua wa jengo hili nikabana, maana watu wanne walikuwa wanazungumza hapo nje na kulikuwa na magari mawili.
Niliposogea nilisikia mtu mmoja anazungumza.
"Hay Shuta, zungumza na mzee halafu utatukuta Sliver Sands marquuis Du Zaire wanapiga huko mpaka saa kumi. Baada ya kazi ngumi namna hii mtu inambidi astarehe kidogo".
"Sawa Mlambo, ngoja nizungumze na mzee nimpe taarifa yote ilivyo halafu nitampitia msichana wangu na mnamo saa tano hivi nitakuwa huko", alijibu Shuta.
"Oke tutaonana", alijibu Mlambo.
Kisha Mlambo na wenzake wakaingia ndani ya gari aina ya Peugeot 504 na walipotokeza kwenye mlango nikaona namba zao TZ 66500. Shuta alirudi na kuingia nyumbani. Mimi niliruka kama paka nikatua ndani ya ua. Baada ya kutua nikasikia viatu vinatembea kwa nje. nikarudi haraka haraka nikabana ndani ya ua wa michongoma. Nilipoangalia nikaona alikuwa ni askari wa usiku aliyekuwa analinda ile nyumba. Bila kuniona alizunguka kunipita kwenye upande huu wa kulia wa nyumba. Nyumba yenyewe iliwa kushoto mwa barabara kama unatoka mjini.
Alipotangulia tu mimi nilimnyemelea bila yeye kunisikia. Nilipokuwa karibu nae nilimrukia na kumtia kabali, taratibu na bila kupiga kelele nilimnyonga na kuhakikisha amekufa kisha nilimsogeza pembeni kwenye giza la michongoma. Kisha nilizunguka nyumba kuangalia hali ilivyo. Nyumba yenyewe ilikuwa na vyumba vitatu vya kulala. Kulikuwa na chumba kimoja kikubwa nikajua hiki ndicho mwenye nyumba alikuwa akilala. Madirisha yalikuwa yamefungwa. Nikatoa pete yangu yenye jiwe la almasi, nikakata tundu katika kioo kisha nikaingia mkono karibu na mahali pa kufungulia dirisha. Baada ya kufungua dirisha la kioo, kulikuwa na dirisha jingine la wavu wa kuzuia mbu. Nilichukua mkasi nikakata sehemu kiasi cha kupitisha mkono karibu na mahali pa kufungulia nikalifungua.
Nilipanda na kutumbukia ndani ya chumba cha kulala kilichokuwa na bafu ndani yake. Nilifunga madirisha vizuri nikaacha mapazia kama yalivyokuwa yamekunjwa. Nilinyata mpaka kwenye mlango nikasikia mtu anasema kwenye simu.
"Hallo naomba mzee. nimepiga karibu dakika tano nzima sipati namba hiyo. Mimi Shuta hapa.
Nilisubiri pale kwenye mlango wa kutokea sebuleni.
"Hallo, Shuta hapa".
Mambo hayakwenda vizuri sana yule msichana ni mpiganaji wa karate na judo sijawahi kuona. Ameua vijana wetu wanne, watatu aliwaua kabla ya kuchomwa kisu, lakini hata wakati amekwisha kuchomwa kisu alimwua Shilonda kwa kumvunja shingo. Lakini hata hivyo nimemwua.
"Nina uhakika kabisa amekufa palepale maana nilimchoma kisu kwenye moyo hasa".
"Ndio sasa tumebakiza wawili ndipo tunaweza kuanza kupakia".
"Haya asante mzee".
Kisha nilisikia anapiga simu tena. "Hallo Sakina yupo. Shuta hapa".
"Aha kisura jitayarishe nakuja kukupitia twende kamanyola nasikia siku hizi wana mtindo mpya wa 79 Scania LBT III... tutakwenda ukauone".
"Dakika kumi na tano nitakuwa hapo".
"Haya kwaheri".
Akarudisha simu.
Nilijua atakuja chumbani hivyo mimi nilijibanza kwenye ukuta karibu na mlango nikamsubiri maana nilisikia viatu vinakuja. Mkono wa kushoto nilishika bastola na mkono wa kulia kisu kile kilichomwua Veronika.
Alifungua mlango akawasha taa huku akipiga mluzi kisha alifululiza kwenda kwenye kabati la nguo bila hata kuniona. Mimi nilirudisha mlango kwa mguu, ndipo akageuka kuniona. Sijaona mtu anastuka namna hii maana palepale jasho lilimtoka, akataka kukaa chini akashindwa, akaanza kugwaya. Nilifikiri atazirai.
"Kumbe wewe unaona kuuwa wenzako ni rahisi na kumbe wewe mwenyewe unaogopa kifo namna hii".
"Niache niache, mimi ninakujua wewe ni nani, nisamehe".
Kuomba kwake msamaha kulinifanya mimi nikasirike zaidi.
"Kabla sijafikiria kukusamehe nataka kujua kiongozi wenu ni nani?".
"Mimi simjui; mimi ni mtu mdogo tu".
"Si unasema mimi unanijua?".
"Ndiyo nakujua wewe ni Willy Gamba, mpelelezi mkuu wa Afrika. Mimi niliwaambia waaache kama wewe wamekuingiza katika upelelezi lakini walikataa".
"Wakina nani?".
"Akina Mlambo".
"Mlambo ndiye nani?".
"Ndiye mkuu wetu sisi kwa upande wa kuua wapinzani".
"Na yeye ni mwanachama wa SANP?".
Alitoa macho na kushitushwa sana na swali langu hili, kisha nikaona anaanza kutokuwa na mshituko.
"Sitasema maneno zaidi nifanye unavyotaka".
"Ahaa, mimi huwa napenda watu shujaa kama wewe".
Niliweka bastola yangu ndani ya mkoba wake nikaweka kisu vizuri kwenye mkanda nikamfuata. Aliponiona sina silaha akaona ajaribu bahati yake. Palepale aligeuka mbogo na kuanza kunishambulia kwa makonde. Alitupa konde la kwanza nikaliona. Akatupa la pili nikaliona. Akatupa la tatu nikashika mkono wake nikamchukua judo na kumtupa upande mwingine wa chumba akaanguka kama papai bovu. Haraka haraka nikamfuata pale chini nikampiga teke la mbavuni na lingine la tumboni akalainika. Kisha nikamkunja vizuri sana. Nikatoa kisu nikachana shati lake akabaki tumbo wazi.
"Sasa utanieleza. Usiponieleza nitakutumbua matumbo na Sakina hutamwona tena. Niambie nani mkubwa wenu?".
Macho ya kutisha yalimtoka kwa kukiangalia kisu na kuona kuwa nilikuwa sitanii.
"Niache, niache nitakwambia mkubwa wetu ni...
Kabla hajamaliza kusema mlango ulipigwa teke na mtu mmoja akaingia ndani na kabla hajafyatua risasi pale tulipokuwa nilijirusha upande mwingine risasi zake zikanikosa ila zikamwingia Shuta tumboni, na mimi wakati ule ule nikamtupia kisu kilichompata katikati ya koo akaanguka chini huku risasi zinatoka ovyo.
Nilisikia vurumai nyingine sebuleni nikajua wako wengi. Kama umeme nilitoa bastola yangu tayari kukabiliana na matatizo.
"Mashuka umempata?", nilisikia sauti inauliza kwa woga.
"Ndiyo", nilijibu kwa sauti ya chini.
Kabla sijampa nafasi nilijirusha na kujiviringisha ndani ya sebule ambamo nilikuta watu wawili mmoja akiwa na bastola. Na kwa vile hakutegemea hatua kama ile alishikwa na bumbuwazi palepale nikapata nafasi ya kumpiga risasi ya katikati ya paji la uso akaanguka chini. Kabla sijawahi kusimama yule mwingine alipiga teke bastola yangu ikaanguka chini, palepale akanipa teke la tumboni nikaanguka chini. Wakati ule ule nikaona anaangalia kule bastola ya yule mwenzake niliyempiga risasi ilikoangukia na akaruka kuichukua. Mimi nikitumia ujuzi wangu wa miaka mingi nilimwahi wakati ndipo anafikisha vidole vyake kwenye bastola nikampiga kichwa kimoja cha sisimizi akaona nyota na kujiviringisha mbali na bastola. Kwa vile alikuwa tayari amenitia mori nilimfuata wakati naye anasimama. Nikaona anajikunja tayari kupigana karate, mimi nikaona ndipo ananipeleka nyumbani.
"Aisee mlambo-iiiiji mjukuu wa Chaka mwana Zulu fanya kazi yako", alijitia mori.
"Ungekuwa mjukuu wa Chaka ufanye jambo la aibu kama kuwa kibaraka wa Makaburu - tazama Mwafrika asiye na aibu".
Aliruka na kutupa karate nikaikinga kwa mikono. Akatupa tena nami nikaizuia, halafu akageuza mara moja, akanipata, kisha akanipata tena, nikajua huyu alikuwa na ujuzi wa kutosha hivyo mimi ilinibidi nibadili na kujaribu Kung-fu. Na hapo hapo nikasikia mwili mzima unasisimka nikamwingia. Kwa sababu ya hasira na baada ya kukumbuka mauaji ya Veronika chuki kubwa iliniingia hivyo nilitupa wimbi la kwanza nikatupa la pili likampata
la tatu nilipopeleka kiganja changu kikamtoboa chini kidogo ya kifua na kutoka na vipande vya matumbo na vitu vingine vya ndani. Alipiga kelele
"Eeeeeeeeeeeeenakufa, eeeeeeee.
Akaanguka chini akafa.
Nilirudi chumbani nikamkuta Shuta yu hai, anajaribu kusimama lakini anashindwa sababu ya risasi zilizomwingia tumboni. Nilichomoa kisu kutoka kwenye maiti ya yule mtu niliyekuwa nimemchoma kooni nikamfuata.
"Kama ulivyomwua Veronika na mimi nakuua hivyo hivyo, maana nilimwahidi aliponiomba nimlipizie kisasi"
"Nisamehe, nipeleke hospitali".
Kusikia hivi roho ilinichemka, nikamchoma kisu katikati ya moyo huku analia hovyo.
"Kwa heri Shuta, mtaonana sasa hivi na Veronika mbele ya Mungu, ukajibu vizuri kwanini umemwua".
Niligeuka na kumwacha anakufa.
Nilipofika sebuleni tu nikasikia gari linapiga breki pale nje. Niliruka nikachukua bastola yangu na kuokota nyingine hapo sebuleni nikabana karibu na mlango wa kutokea nje nikasubiri.
Mlango ulipigwa teke na hapo hapo wakaingia watu wawili kama risasi, bastola mkononi, wakajiviringisha mmoja akiwa tayari kupambana na kitu chochote mbele yake na mwingine akajiviringisha na kuegeka nyuma. Mimi nilikuwa tayari kwa lolote.
"Ni mimi usiftatue", nilipiga kelele.
Kumbe hawa walikuwa ni Eddy na Sherriff.
Oh Bosi, samahani", Eddy alisema huku akiruka.
"Siku nyingine kutatokea ajali namna hii", nilimwambia.
"Tunaomba isitokee", Sherriff alijibu naye akisimama.
"Umefanya kazi kubwa sana Bosi", Eddy alinipongeza baada ya wao kuangalia maiti zote ndani ya nyumba hii.
"Ninastahili kazi kama hii", nilijibu.
"Sisi tulipongojea kwa muda mrefu tukaona tukufuate baada ya kujua kutoka kwa Zabibu kuwa umekuja huku. Tulihisi kuwa kuchelewa kwako unaweza ukawa katika matatizo. Tulipokuja tulikuta gari lako na gari jingine hapo mbele yameegeshwa. gari lako lilikuwa limetolewa upepo ndani ya tairi zote, hivyo hii ilituhakikishia kuwa uko msambweni", alieleza Eddy huku tukielekea kwenye gari lao. Ndani ya gari nilimkuta Zabibu.
"Oh Willy mpenzi uko salama?".
Alifungua mlango na kunirukia akiweka mikono shingoni mwangu na kunibusu.
"Na wewe umefuata nini?", nilimwuliza.
Nilimkarisha ndani ya gari kwenye viti vya nyuma mimi nikakaa huku Sherriff na Eddy wakaingia mbele, Eddy akatia gari gea tukaondoka.
"Nilikuja nikuone kama ni kufa tufe wote. Maana sijui nini kimeniingia nakuona wewe ndiye mwenzangu sasa. Nikiwa karibu na wewe nasahau yote yaliyopita".
"Usizoee kutembea na sisi mtoto kama wewe, hufai hata kujeruhiwa kidogo. tuachie sisi hatari ndiyo kazi yetu. Sitaki kupatwa mkasa kama niliopatwa nao kwa Veronika".
Kisha nikamweleza toka mwanzo mpaka mwisho wa mapambano yangu nyumbani kwa Shuta.
"Naona huyu Mlambo na wenzake walitia shaka walipoona gari langu. Hivyo walirudi kuhakikisha. Lazima niseme Mlambo alikuwa na mafunzo ya hali ya juu ya jeshi hata mimi alinitoa jasho".
Tulielekea nyumbani kwa Eddy.
ITAENDELEA
USIKU WA HEKAHEKA
Tulipofika Kilimanjaro Hoteli ilikuwa yapata saa tatu kamili. Tulipokuwa njiani kuelekea Kilimanjaro nilimweleza Eddy mambo yote niliyokuwa nimepata toka kwa Zabibu, mambo ambayo hata yeye alisema yalionyesha ufumbuzi wa jambo hili kwa mtu mwenye kufikiri. Tuliingia hotelini tukapanda lifti iliyotushusha orofa ya pili. Tulipotoka ndani ya lifti mara ile hali ya tahadhari ilituingia. Mimi nilitoa bastola yangu nikaiweka tayari na Eddy akafanya vile vile.
Tulipofika mlango wa chumba namba 206 tulikuta umefungwa, niligonga nikiwa nimesimama upande kabisa. Niligonga mlango mara mbili haraka haraka, halafu nikatulia kidogo kisha nikagonga tena, kwani hivi ndivyo Veronika alikuwa amenielekeza namna ya kujitambulisha lakini sikusikia kitu. Nilimonyesha ishara Eddy abane ukutani wakati mimi nafungua.
Nilifungua mlango ghafla. Tishio nililolikuta sijawahi kulipata tena, kwani Veronika alikuwa amelala kwenye sofa na kisu chenye mpini mwekundu kikiwa kimemwingia juu kidogo ya titi la kushoto. Kidogo ningezimia lakini nilijikaza nikakimbia pale kwenye sofa huku nikikanyaga maiti za watu wengine hapo chumbani.
Veronika alikuwa bado ameshikilia mkono wa simu mikononi mwake. Nilipomfikia nilimkuta bado yuko hai. Wakati huo Eddy nae alikuwa ameingia akanipa glasi ya whiski.
"Bosi jikaze, mnyweshe hii whiski mimi naita gari la hospitali"'
Nilimnywesha Veronika kisha nikamtingisha akafunua macho akapata fahamu kidogo.
"Vero, Willy hapa, niambie nani amefanya hivi".
"Walikuja.... watatu... nikapam...bana ...nikawaua nikakupigia simu.... ku...ku...kumbe walikuwepo... wengine ...wawili ... mmoja ... akamwita ... Shu... Shu...Shuta muue.... mimi kugeuka ... akanichoma... ki... kisu... nikawahi ...kumpiga yule mwingine ...kwa... akafa... Shuta... akakimbia ...nika...
Hakuweza kusema tena. Nikamwongeza whiski na kumtingisha.
"Oh Vero, nimeita gari la wagonjwa na mganga anakuja sasa hivi utapona tu.
"Si...siwezi...nitakufa...nimekufa...ame...moyo...Willy na...nakufa...na...ku...penda ...hakuna tena... mwanamume... niliye... mpenda...kama wewe. Ni...nimefurahi...kukuona ...ma...mara... ya...mwisho...nikifa ...kwa ajili ya Afrika... siogopi...kufa...kwani nimekufa ...kwa sa...sabab...bu...nzuri. Ende...le..za ...ma...pa...mba...no... Willy ...Mungu...a...ku...sai...die...uni...ku...pi...zie...kisasi Afrika. Ni...busu...na... ku...
Nilijua Veronika hawezi kuchukua dakika moja zaidi, niliweka midomo yangu kwenye midomo yake na kulamba damu yake ambayo sasa ilikuwa inatoka mdomoni.Alitabasamu na macho yake yakang'ara kiasi ambacho sikuwahi kuyaona yanang'ara vile halafu akayapepesa akafariki. Alikufa huku akitabasamu.
Sikuwahi kulia na kupata uchungu kama wakati wa kifo cha Veronika. Nilijilaumu. Kama ningekwenda nae kwa Zabibu asingekufa.
Eddy alinikuta nabubujika machozi kama mama anayemlilia mtoto wake wa pekee.
"Bosi jikaze", Eddy alinishauri.
"Washenzi hawa, nduli hawa, watanitambua. Kwanini Mungu anaruhusu mtu kama Veronika kufa mikononi mwangu?. Eee Mungu nisaidie nilipize kisasi kwa ajili ya mwanamapinduzi huyu wa Afrika nzima", niliomba kwa sauti huku machozi yananitoka. Vero alikuwa amekufa kishujaa. Alikuwa amewaua maadui wanne pale pale chumbani.
Niling'oa kile kisu nikasafisha damu yake kwenye nguo zake.
"Kisu hiki hiki kitawauwa kama walivyomwua Veronika", nilisema.
"Bosi ninataka toka sasa tuwe pamoja".
"Hapana sasa hivi, fanya mpango wa kuondoa maiti hizi humu ndani. Na umwarifu Chifu, polisi wala wakuu wa hoteli wasiingilie. Na halafu kampashe Sherriff habari hizi za huzuni. Muushughulikie mwili wa Veronika uweze kupelekwa kwao. Mwambie Sherriff ashughulike na habari hiyo tu mambo mengine aniachie. Mwambie Chifu mambo yote yalivyo mpaka sasa mimi namfuata Shuta lazima alipe. Fanya hayo kwanza halafu nitakapokuhitaji nitakujulisha".
Niliondoka na kumwacha Eddy mle ndani ya chumba nikakimbia kwenye lifti iliyonitelemsha chini. Nilipita pale mapokezi huku nikikimbia kiasi cha watu wote kunishangaa.
Niliingia ndani ya gari Eddy alilokuwa amekodi na kuliacha Kilimanjaro Hoteli nikaondoka kwenda kumtafuta Shuta.
II
Niliondoka na kuelekea nyumbani kwa Eddy nilikomwacha Zabibu. Njiani nilifikiria uhusiano wangu na Veronika tokea siku tuliyoonana mwenye ndege mpaka kifo chake kilipotokea mikononi mwangu dakika chache zilizopita. Nilisikia uchungu usio kifani. Hasira na chuki yangu kwa makaburu, mabeberu na vibaraka wao ilizidi kiwango chake cha kila siku.
"Kifo peke yake ndicho kitaniachisha kuwawinda hawa wadhalimu maishani mwangu", niliapa.
Nilipofika nyumbani kwa Eddy nilimkuta Zabibu amekaa kwenye sofa pale tulipomwacha.
"Kumetokea nini, mbona ulikuwa unalia?", Zabibu aliniuliza baada ya kuniangalia kwa muda mfupi.
Nilimweleza yaliyompata Veronika, na jinsi urafiki wetu na Veronika ulivyokuwa umekomaa tangu kuonana mwenye ndege wakati tukielekea Freetown. Hakika nilijuta kumfahamu Veronika afadhali nisingeonana nae.
"Usisikitike sana, sasa tunakuwa watu wawili tuliopoteza marafiki zetu. Lililopo sasa ni sisi kutiana moyo na kusaidiana kuwatafuta hawa waliofanya matendo haya.
Nilijisikia vizuri kidogo Zabibu kuwa pamoja nami.
"Unajua Shuta anapokaa?", niliuliza.
"Ndio, anakaa Oysterbay, Kaunda Drive No. 11230".
"Basi, sasa wewe tulia hapa mimi nitarudi muda si mrefu".
"Twende sote".
"Hapana. Kazi hii huijui niachie mimi, wewe pumzika hapa. Ukiona usingizi chumba hicho hapo kalale. Tutaonana baadaye".
"Lakini jihadhari inaonekana watu hawa ni hatari kabisa, sitapenda kusikia umeuawa, nikisikia tu na mimi nitajiua", aliniambia Zazibu akionyesha hali ya mapenzi kama kwamba tumekuwa marafiki siku nyingi.
Mimi huwa sielewi kwa nini binadamu hawa hutokea kunipenda mara tu nionyeshapo uso wangu. Niliondoka na kuelekea Oysterbay. Niliingia Kaunda Drive na kuanza kuangalia namba za nyumba. Niliendesha polepole mpaka nikaona nyumba. Nilipokuwa napita mbele ya lango la nyumba hiyo mlango wa mbele ulifunguliwa mimi nikaendelea mbele kidogo nikaegesha gari langu, halafu nikarudi kwa miguu.
Nilipofika kwenye ua wa jengo hili nikabana, maana watu wanne walikuwa wanazungumza hapo nje na kulikuwa na magari mawili.
Niliposogea nilisikia mtu mmoja anazungumza.
"Hay Shuta, zungumza na mzee halafu utatukuta Sliver Sands marquuis Du Zaire wanapiga huko mpaka saa kumi. Baada ya kazi ngumi namna hii mtu inambidi astarehe kidogo".
"Sawa Mlambo, ngoja nizungumze na mzee nimpe taarifa yote ilivyo halafu nitampitia msichana wangu na mnamo saa tano hivi nitakuwa huko", alijibu Shuta.
"Oke tutaonana", alijibu Mlambo.
Kisha Mlambo na wenzake wakaingia ndani ya gari aina ya Peugeot 504 na walipotokeza kwenye mlango nikaona namba zao TZ 66500. Shuta alirudi na kuingia nyumbani. Mimi niliruka kama paka nikatua ndani ya ua. Baada ya kutua nikasikia viatu vinatembea kwa nje. nikarudi haraka haraka nikabana ndani ya ua wa michongoma. Nilipoangalia nikaona alikuwa ni askari wa usiku aliyekuwa analinda ile nyumba. Bila kuniona alizunguka kunipita kwenye upande huu wa kulia wa nyumba. Nyumba yenyewe iliwa kushoto mwa barabara kama unatoka mjini.
Alipotangulia tu mimi nilimnyemelea bila yeye kunisikia. Nilipokuwa karibu nae nilimrukia na kumtia kabali, taratibu na bila kupiga kelele nilimnyonga na kuhakikisha amekufa kisha nilimsogeza pembeni kwenye giza la michongoma. Kisha nilizunguka nyumba kuangalia hali ilivyo. Nyumba yenyewe ilikuwa na vyumba vitatu vya kulala. Kulikuwa na chumba kimoja kikubwa nikajua hiki ndicho mwenye nyumba alikuwa akilala. Madirisha yalikuwa yamefungwa. Nikatoa pete yangu yenye jiwe la almasi, nikakata tundu katika kioo kisha nikaingia mkono karibu na mahali pa kufungulia dirisha. Baada ya kufungua dirisha la kioo, kulikuwa na dirisha jingine la wavu wa kuzuia mbu. Nilichukua mkasi nikakata sehemu kiasi cha kupitisha mkono karibu na mahali pa kufungulia nikalifungua.
Nilipanda na kutumbukia ndani ya chumba cha kulala kilichokuwa na bafu ndani yake. Nilifunga madirisha vizuri nikaacha mapazia kama yalivyokuwa yamekunjwa. Nilinyata mpaka kwenye mlango nikasikia mtu anasema kwenye simu.
"Hallo naomba mzee. nimepiga karibu dakika tano nzima sipati namba hiyo. Mimi Shuta hapa.
Nilisubiri pale kwenye mlango wa kutokea sebuleni.
"Hallo, Shuta hapa".
Mambo hayakwenda vizuri sana yule msichana ni mpiganaji wa karate na judo sijawahi kuona. Ameua vijana wetu wanne, watatu aliwaua kabla ya kuchomwa kisu, lakini hata wakati amekwisha kuchomwa kisu alimwua Shilonda kwa kumvunja shingo. Lakini hata hivyo nimemwua.
"Nina uhakika kabisa amekufa palepale maana nilimchoma kisu kwenye moyo hasa".
"Ndio sasa tumebakiza wawili ndipo tunaweza kuanza kupakia".
"Haya asante mzee".
Kisha nilisikia anapiga simu tena. "Hallo Sakina yupo. Shuta hapa".
"Aha kisura jitayarishe nakuja kukupitia twende kamanyola nasikia siku hizi wana mtindo mpya wa 79 Scania LBT III... tutakwenda ukauone".
"Dakika kumi na tano nitakuwa hapo".
"Haya kwaheri".
Akarudisha simu.
Nilijua atakuja chumbani hivyo mimi nilijibanza kwenye ukuta karibu na mlango nikamsubiri maana nilisikia viatu vinakuja. Mkono wa kushoto nilishika bastola na mkono wa kulia kisu kile kilichomwua Veronika.
Alifungua mlango akawasha taa huku akipiga mluzi kisha alifululiza kwenda kwenye kabati la nguo bila hata kuniona. Mimi nilirudisha mlango kwa mguu, ndipo akageuka kuniona. Sijaona mtu anastuka namna hii maana palepale jasho lilimtoka, akataka kukaa chini akashindwa, akaanza kugwaya. Nilifikiri atazirai.
"Kumbe wewe unaona kuuwa wenzako ni rahisi na kumbe wewe mwenyewe unaogopa kifo namna hii".
"Niache niache, mimi ninakujua wewe ni nani, nisamehe".
Kuomba kwake msamaha kulinifanya mimi nikasirike zaidi.
"Kabla sijafikiria kukusamehe nataka kujua kiongozi wenu ni nani?".
"Mimi simjui; mimi ni mtu mdogo tu".
"Si unasema mimi unanijua?".
"Ndiyo nakujua wewe ni Willy Gamba, mpelelezi mkuu wa Afrika. Mimi niliwaambia waaache kama wewe wamekuingiza katika upelelezi lakini walikataa".
"Wakina nani?".
"Akina Mlambo".
"Mlambo ndiye nani?".
"Ndiye mkuu wetu sisi kwa upande wa kuua wapinzani".
"Na yeye ni mwanachama wa SANP?".
Alitoa macho na kushitushwa sana na swali langu hili, kisha nikaona anaanza kutokuwa na mshituko.
"Sitasema maneno zaidi nifanye unavyotaka".
"Ahaa, mimi huwa napenda watu shujaa kama wewe".
Niliweka bastola yangu ndani ya mkoba wake nikaweka kisu vizuri kwenye mkanda nikamfuata. Aliponiona sina silaha akaona ajaribu bahati yake. Palepale aligeuka mbogo na kuanza kunishambulia kwa makonde. Alitupa konde la kwanza nikaliona. Akatupa la pili nikaliona. Akatupa la tatu nikashika mkono wake nikamchukua judo na kumtupa upande mwingine wa chumba akaanguka kama papai bovu. Haraka haraka nikamfuata pale chini nikampiga teke la mbavuni na lingine la tumboni akalainika. Kisha nikamkunja vizuri sana. Nikatoa kisu nikachana shati lake akabaki tumbo wazi.
"Sasa utanieleza. Usiponieleza nitakutumbua matumbo na Sakina hutamwona tena. Niambie nani mkubwa wenu?".
Macho ya kutisha yalimtoka kwa kukiangalia kisu na kuona kuwa nilikuwa sitanii.
"Niache, niache nitakwambia mkubwa wetu ni...
Kabla hajamaliza kusema mlango ulipigwa teke na mtu mmoja akaingia ndani na kabla hajafyatua risasi pale tulipokuwa nilijirusha upande mwingine risasi zake zikanikosa ila zikamwingia Shuta tumboni, na mimi wakati ule ule nikamtupia kisu kilichompata katikati ya koo akaanguka chini huku risasi zinatoka ovyo.
Nilisikia vurumai nyingine sebuleni nikajua wako wengi. Kama umeme nilitoa bastola yangu tayari kukabiliana na matatizo.
"Mashuka umempata?", nilisikia sauti inauliza kwa woga.
"Ndiyo", nilijibu kwa sauti ya chini.
Kabla sijampa nafasi nilijirusha na kujiviringisha ndani ya sebule ambamo nilikuta watu wawili mmoja akiwa na bastola. Na kwa vile hakutegemea hatua kama ile alishikwa na bumbuwazi palepale nikapata nafasi ya kumpiga risasi ya katikati ya paji la uso akaanguka chini. Kabla sijawahi kusimama yule mwingine alipiga teke bastola yangu ikaanguka chini, palepale akanipa teke la tumboni nikaanguka chini. Wakati ule ule nikaona anaangalia kule bastola ya yule mwenzake niliyempiga risasi ilikoangukia na akaruka kuichukua. Mimi nikitumia ujuzi wangu wa miaka mingi nilimwahi wakati ndipo anafikisha vidole vyake kwenye bastola nikampiga kichwa kimoja cha sisimizi akaona nyota na kujiviringisha mbali na bastola. Kwa vile alikuwa tayari amenitia mori nilimfuata wakati naye anasimama. Nikaona anajikunja tayari kupigana karate, mimi nikaona ndipo ananipeleka nyumbani.
"Aisee mlambo-iiiiji mjukuu wa Chaka mwana Zulu fanya kazi yako", alijitia mori.
"Ungekuwa mjukuu wa Chaka ufanye jambo la aibu kama kuwa kibaraka wa Makaburu - tazama Mwafrika asiye na aibu".
Aliruka na kutupa karate nikaikinga kwa mikono. Akatupa tena nami nikaizuia, halafu akageuza mara moja, akanipata, kisha akanipata tena, nikajua huyu alikuwa na ujuzi wa kutosha hivyo mimi ilinibidi nibadili na kujaribu Kung-fu. Na hapo hapo nikasikia mwili mzima unasisimka nikamwingia. Kwa sababu ya hasira na baada ya kukumbuka mauaji ya Veronika chuki kubwa iliniingia hivyo nilitupa wimbi la kwanza nikatupa la pili likampata
la tatu nilipopeleka kiganja changu kikamtoboa chini kidogo ya kifua na kutoka na vipande vya matumbo na vitu vingine vya ndani. Alipiga kelele
"Eeeeeeeeeeeeenakufa, eeeeeeee.
Akaanguka chini akafa.
Nilirudi chumbani nikamkuta Shuta yu hai, anajaribu kusimama lakini anashindwa sababu ya risasi zilizomwingia tumboni. Nilichomoa kisu kutoka kwenye maiti ya yule mtu niliyekuwa nimemchoma kooni nikamfuata.
"Kama ulivyomwua Veronika na mimi nakuua hivyo hivyo, maana nilimwahidi aliponiomba nimlipizie kisasi"
"Nisamehe, nipeleke hospitali".
Kusikia hivi roho ilinichemka, nikamchoma kisu katikati ya moyo huku analia hovyo.
"Kwa heri Shuta, mtaonana sasa hivi na Veronika mbele ya Mungu, ukajibu vizuri kwanini umemwua".
Niligeuka na kumwacha anakufa.
Nilipofika sebuleni tu nikasikia gari linapiga breki pale nje. Niliruka nikachukua bastola yangu na kuokota nyingine hapo sebuleni nikabana karibu na mlango wa kutokea nje nikasubiri.
Mlango ulipigwa teke na hapo hapo wakaingia watu wawili kama risasi, bastola mkononi, wakajiviringisha mmoja akiwa tayari kupambana na kitu chochote mbele yake na mwingine akajiviringisha na kuegeka nyuma. Mimi nilikuwa tayari kwa lolote.
"Ni mimi usiftatue", nilipiga kelele.
Kumbe hawa walikuwa ni Eddy na Sherriff.
Oh Bosi, samahani", Eddy alisema huku akiruka.
"Siku nyingine kutatokea ajali namna hii", nilimwambia.
"Tunaomba isitokee", Sherriff alijibu naye akisimama.
"Umefanya kazi kubwa sana Bosi", Eddy alinipongeza baada ya wao kuangalia maiti zote ndani ya nyumba hii.
"Ninastahili kazi kama hii", nilijibu.
"Sisi tulipongojea kwa muda mrefu tukaona tukufuate baada ya kujua kutoka kwa Zabibu kuwa umekuja huku. Tulihisi kuwa kuchelewa kwako unaweza ukawa katika matatizo. Tulipokuja tulikuta gari lako na gari jingine hapo mbele yameegeshwa. gari lako lilikuwa limetolewa upepo ndani ya tairi zote, hivyo hii ilituhakikishia kuwa uko msambweni", alieleza Eddy huku tukielekea kwenye gari lao. Ndani ya gari nilimkuta Zabibu.
"Oh Willy mpenzi uko salama?".
Alifungua mlango na kunirukia akiweka mikono shingoni mwangu na kunibusu.
"Na wewe umefuata nini?", nilimwuliza.
Nilimkarisha ndani ya gari kwenye viti vya nyuma mimi nikakaa huku Sherriff na Eddy wakaingia mbele, Eddy akatia gari gea tukaondoka.
"Nilikuja nikuone kama ni kufa tufe wote. Maana sijui nini kimeniingia nakuona wewe ndiye mwenzangu sasa. Nikiwa karibu na wewe nasahau yote yaliyopita".
"Usizoee kutembea na sisi mtoto kama wewe, hufai hata kujeruhiwa kidogo. tuachie sisi hatari ndiyo kazi yetu. Sitaki kupatwa mkasa kama niliopatwa nao kwa Veronika".
Kisha nikamweleza toka mwanzo mpaka mwisho wa mapambano yangu nyumbani kwa Shuta.
"Naona huyu Mlambo na wenzake walitia shaka walipoona gari langu. Hivyo walirudi kuhakikisha. Lazima niseme Mlambo alikuwa na mafunzo ya hali ya juu ya jeshi hata mimi alinitoa jasho".
Tulielekea nyumbani kwa Eddy.
ITAENDELEA
Subscribe to:
Posts (Atom)